Samatta na Victor Wanyama watemwa na CAF
Awali CAF ilitangaza majina 30 ya wachezaji watakaowania tuzo hiyo huku Mbwana Samatta pamoja na Victor Wanyama wa klabu ya Tottenham, Yannick Bolasie wa DR Congo anayechezea Everton na wengine walikuwa ni miongoni kati ya wachezaji waliotajwa kuwania tuzo hiyo.
Wachezaji wengine waliotajwa kuwania tuzo ya mchezaji bora wa Afrika kwa wanaocheza ligi za Afrika ni pamoja na Khama Billiat wa Mamelodi Sundowns (Zimbabwe), Keegan Dolly wa Mamelodi Sundowns (South Africa), Rainford Kalaba wa TP Mazembe (Zambia), Hlompho Kekana wa Mamelodi Sundowns (South Africa) na Denis Onyango wa Mamelodi Sundowns (Uganda).
Tuzo hizo zitatolewa Alhamisi ya Januari 5 mwakani mjini Abuja, Nigeria.
Comments
Post a Comment