Ndege iliyobeba wachezaji wa Brazil yaanguka Colombia
Maelezo kamili ya ajali hiyo hayajafahamika lakini habari zinasema kwamba kuna watu 6 walionusurika.
Ndege hiyo ya kukodisha iliyokuwa ikitokea Bolivia, ilikuwa na timu ya soka ambayo ilikuwa icheze katika fainali ya Kombe la Amerika ya Kusini dhidi ya timu ya Atletico Nacional ya Medellin. Hivyo, fainali hiyo imeahirishwa.
Ripoti zinasema ndege hiyo yenye leseni namba CP 2933, iliyoanguka muda mfupi kabla ya saa sita usiku, ilielezewa na Meya wa Medellin, Federico Gutierrez, kama “janga kubwa”, akiongeza kwamba inawezekana kuna watu walionusurika.
Comments
Post a Comment