Jeshi la Polisi Morogoro lathibitisha kumshikilia Nay wa Mitego

Image result for ney wa mitego
Msanii wa muziki wa Bongo Fleva Nay Wa Mitego amekamatwa na Jeshi la Polisi wilayani Mvomero, Morogoro alikokuwa ameenda kwaajili ya kutumbuiza.
Nay wa mitego amethibitisha kushikiliwa kwake kupitia ukurasa wake wa Instagram:
“Nimekamatwa kweli. Muda Huu nikiwa hotel Morogoro baada ya kumaliza Kazi yangu iliyo ni leta. Napelekwa Mvomelo Police.
Nawapenda Watanzania wote.”
Polisi Morogoro wamethibitisha kumshikilia “Ni kweli tunamshikilia Nay wa Mitego, tulipewa maelekezo tumtafute baada ya kutorokea Dodoma
Mpaka sasa bado haijafahamika sababu ya kukamatwa kwake.

Comments

Popular Posts